Home » » JAMANI TUWE NA HURUMA

JAMANI TUWE NA HURUMA



Kundi lisilo na fursa ya elimu kwa kubakwa, kulawitiwa ndiyo maisha -2
Ombaomba wakiwa na watoto wao katika eleo la Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam 
Kwa ufupi
Utafiti wa  Shirika la Mkombozi mwaka 2005, unataja sababu za watoto wa mitaani kuongezeka kuwa ni  wakinababa kutelekeza familia.
  1. *Ndoa nyingi kuvunjika na familia kuongozwa na mzazi mmoja.
  2. *Kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaozaliwa nje ya ndoa.
  3. *Watu kuzaa watoto wengi wasioweza kuwalea
Wanakuja usiku kwenye maeneo tunayolala wanatafuta wanayemtaka ili akawafanye, ukimaliza wanakupa hela na wengine wanakunyima wanakufukuza
Juma lililopita tuliona jinsi watoto waishio mitaani wanavyokosa fursa ya elimu na kuambulia mateso ikiwa pamoja na kulala nje, kulawitiwa, kubakwa na kukosa mahitaji muhimu kama chakula na mavazi.
Wiki hii, watoto hao wanaendelea simulizi la madhila mbalimbali yanayowakuta katika mazingira hayo magumu, huku Serikali ikiainisha mikakati ya kukabilina na hali hiyo.
Watoto kulawitiwa
Mwananchi iliwahi kufanya uchunguzi juu ya maisha ya vijana hao na kubaini kuwa, wengi hulazimishwa kulawitiwa ama kulawiti.
 “Wanakuja usiku kwenye maeneo tunayolala wanatafuta wanayemtaka ili akawafanye, wakimaliza wanakupa hela na wengine wanakunyima wanakufukuza,” anasema mmoja wa watoto hao.
Watoto hawa, licha ya matatizo wanayokutana nayo, wakati mwingine huonekana kama wasiostahili kuonekana machoni mwa baadhi ya watu, hasa viongozi wa kitaifa.
Mtoto mwingine akieleza masaibu yake huku akibubujikwa na machozi anasema  siku ya nne tangu aingie Dar es Salaam akitokea kwao, Dodoma alikuwa  amelala  kwenye kibaraza cha jengo la Soko la Kariakoo, alianza kusikia maumivu  makali sehemu za haja kubwa, aliposhtuka alijikuta katika mikono na mwanamume aliyemwita mzee ambaye alikuwa akimlawiti.
 “Nilitaka kupiga kelele, lakini alikuwa ameniziba mdomo na amenielekeza sehemu ya ukutani, alikuwa amechukua maboksi mengi akawa ameyaweka yametufunika kabisa, haikuwa rahisi kwa mtu kuona kilichokuwa kikifanyika. Kwa hiyo nikashindwa kumfanya chochote, alipomaliza akaniambia nikipiga kelele ataniua,” anaeleza na kuongeza:
 “Baada ya kunifanya vile sikuweza kulala tena siku ile, kama baada ya wiki kupita, yule mzee alikuja tena na kunikamata kwa nguvu na kuniingiliia tena nikiwa tena nimelala.Sasa ikawa ndiyo tabia yake mpaka ikabidi mimi nihame lile eneo nikaja huku Uhindini.”
Mbali na mzee huyo, mtoto huyo anasema pia kwa nyakati tofauti amewahi kukamatwa na vijana wenzake wanaoishi mitaani ambao ni wakubwa na wakamlawiti.
Watoto wengine wanasema kwamba, baadhi ya watu hufika kwenye maeneo wanapoishi na kusema wanataka kuwapeleka shule, kinyume na wanavyosema huwachukua na kwenda kuwalazimisha kufanya
Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc