Home » » HABARI MBALIMBALI ZA WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA KUTOKA BUNGENI DODOMA

HABARI MBALIMBALI ZA WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA KUTOKA BUNGENI DODOMA

HABARI MBALIMBALI ZA WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA KUTOKA BUNGENI DODOMA



KILIMO KUTUMIA SHS. 328,134,608,000 KATIKA MWAKA WA FEDHA UJAO
Habariz zote za Bunge na Benedict Liwenga-Maelezo, Dodoma.
Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika inatarajia kutumia jumla ya shilingi 328,134,608,000/- katika mwaka ujao wa fedha.

Takwimu hizo zimetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza wakati akiwasilisha Bungeni Makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka 2013/14.

Alisema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi 247,094,320,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya kawaida na Shilingi 81,040,288,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya maendeleo.

Chiza aliongeza kuwa  Shilingi 210,175,943,000 ni kwa ajili ya Matumizi Mengine (OC) kwa ajili ya Wizara hiyo .

Aidha ,shilingi 25,602,969,000 ni kwa ajili ya Mishahara (PE) ya Wizara na Shilingi11,315,408,000 ni Mishahara (PE) ya Bodi na Taasisi zote zilizoko chini ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.

Kwa upande shughuli za maendeleo, Chiza alisema kuwa Wizara hiyo imetenga kiasi cha shilingi 23,927,000,000 ikiwa ni fedha za ndani na shilingi 57,113, 288,000 ni fedha za Nje.

Wabunge wanatarajia kujadili bajeti ya Wizara ya Kilimo , Chakula na Ushirika kwa kipindi cha siku mbili ambapo itahitimishwa kesho.

Katika hatua nyingine Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Mhe. Chiza amesema Serikali inatarajia kufufua Kituo cha Kilimo Anga ili kukiwezesha kuwa na ndege na Wataalam watakaosaidia kudhibiti milipuko ya visumbufu vya mazao hasa Nzige.

Mhe. Chiza amesema kwa kiasi kikubwa Serikali imekuwa ikitegemea huduma ya ndege kukodi kutoka kwenye mashirika ya kikanda ya kudhibiti nzige wekundu na nzige wa jangwani ambazo wakati mwingine hazipatikani wakati zinazohitajika.

Kufuatia hali hiyo amesema Wizara katika mwaka wa fedha 2012/13 imekamilisha viwango vya kiufundi (Technical Specifications) kwa ajili ya kutangaza zabuni ya ununuzi wa ndege moja ya kunyunyuzia viuatilifu.
Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc