Home » » SERIKALI: VIJANA SASA KUJIAJIRI KATIKA KILIMO CHA KIBIASHARA

SERIKALI: VIJANA SASA KUJIAJIRI KATIKA KILIMO CHA KIBIASHARA

SERIKALI: VIJANA SASA KUJIAJIRI KATIKA KILIMO CHA KIBIASHARA

2
MH. Waziri Chiza

Na Boniphace Nyabweta, Maelezo Dodoma.

 Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika imekamilisha andiko la namna ya kuwavutia vijana kujiajiri katika kilimo cha biashara.
Akiwasilisha Makadirio na Matumizi ya Wizara yake kwa mwaka wa fedha 2013/14, Waziri Chiza amesema kuwa andiko hilo litatumika kuandaa mipango ya kuwezesha vijana kujiajiri katika kilimo kwa kushirikisha wadau wote.
 Wakati program hiyo inakamilishwa , tayari baadhi ya vijana wamekwishaanza kujiajiri katika kilimo katika mikoa mbalimbali hapa nchini.
 Mhe. Chiza amebainisha kuwa katika kijiji cha Isaka-Malilo-Igunga wahitimu 10 wa Vyuo Vikuu mbalimbali hapa nchini wamejiunga pamoja na tayari wamepewa ekari 150 wanazozitumia kulima zao la alizeti kibiashara.
“Wizara imewezesha kwa kuwapatia chakula na pampu mbili kwa ajili ya umwagiliaji”, alisema Mhe. Chiza.
 Alitaja kikundi kingine kuwa kipo  Arusha,ambacho ni cha mtandao wa wakulima 1000 cha “Home Vegetable Group” wanaozalisha mboga mboga na mahindi machanga .
 Aidha,Waziri Chiza amebainisha kuwa katika mkoa wa Singida, kikundi cha Vijana kimewezeshwa kulima alizeti kibiashara ambapo wamepatiwa eneo la hekta 200 kwa ajili ya shughuli hizo na mkoani Kigoma wilayani Kibondo kikundi cha vijana wanaolima muhogo kibiashara wamewezeshwa.
Waziri amesema, Wizara yake kupitia DASIP imetoa mafunzo ya kilimo na ufugaji bora kwa vijana 179,698 na kuwawezesha kupata ajira katika miradi ya jamii, teknolojia za kilimo na mifugo na kuanzisha mashamba na ufugaji.
 “Kati ya vijana hao 1,669 wameajiriwa kwenye miradi ya jamii, 1,043 katika miradi ya teknolojia ya kilimo na 178,986 wameanzisha mashamba ya kilimo na ufugaji bora”. Mhe. Chiza alisema.


BONIPHACE NYABWETA NI MWANDISHI WA HABARI WA KUJITEGEMEA NA KUPITIA BLOG HII NINA IMANI TUTAWEZA KUPEANA HABARI MBALIMBALI ZA KILIMO, TEKNOLOJIA NA BURUDANI ZITAKAZOFURAHISHA NA KUELIMISHA NAOMBA USHIRIKIANO WENU ILI TUWEZE KUFIKA TULIPOKUSUDIA

Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc