Home » » IDN/YFCC KUTOA TUZO KWA WAKULIMA BORA NA TAASISI ZILIZOSAIDIA WAKULIMA SIKU YA NANE NANE WILAYA YA NZEGA

IDN/YFCC KUTOA TUZO KWA WAKULIMA BORA NA TAASISI ZILIZOSAIDIA WAKULIMA SIKU YA NANE NANE WILAYA YA NZEGA

Na: Protas Charle

Taasisi isiyo ya Kiserikali INFORMATION FOR DISSEMINATION NETWORK (IDN) inayofanya kazi Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora, kupitia mradi wa kuwezesha vijana kujiajiri YOUTH FOR CHANGE kupitia fursa ya Kilimo na Teknolojia ya habari na mawasiliano, imeandaa tuzo kwa wakulima, wafugaji na taasisi zilizosaidia wakulima wa Wilaya ya Nzega.

Tuzo hizo zitatolewa siku ya sikukuu ya wakulima maarufu kama nanenane ambapo taasisi hiyo imeamua kuthamini mchango wa wakulima wadogo wa Wilaya ya Nzega ili kuwapa hamasa ya kuendelea kujikita zaidi katika kilimo cha biashara na kuondokana na kilimo cha mazao ya chakula pekee.

Akizungumza katika mahojiano na wanahabari wa taasisi hiyo inayojishughulisha na usambazaji wa habari kwa jamii, Mratibu wa Mradi Ndugu Boniphace Nyabweta, alisema taasisi yake kupitia mradi wa kuwezesha vijana kujiajiri kupitia kilimo na teknolojia ya habari na mawasiliano wameamua kuandaa Tuzo kwa lengo la kuwakutanisha wakulima, wafugaji na taasisi zilizosaidia wakulima wa Wilaya ya Nzega katika kipindi cha mwaka 2012/2013.

Aidha, mratibu alisema kutokana na vijana walio katika mradi wa Youth for Change, kutekeleza mradi wa Kilimo na Teknolojia ya habari na mawasiliano, itasaidia wakulima wa Wilaya ya Nzega kujifunza mambo mbalimbali yatakayo wasilishwa katika sherehe hizo za utoaji tuzo na kupata taarifa za kilimo, upatikanaji wa pembejeo za kilimo, masoko, mikopo na kuwasilisha kero wanazozipata katika kazi zao kwa viongozi wa Serikali ili zishughulikiwe.
Alisema mgeni rasmi katika utoaji wa tuzo hizo atakuwa Afisa Kilimo wa Wilaya ambapo ataambatana na watendaji wengine toka katika idara ya kilimo na mifugo wa halmashauri ya Nzega na viongozi wa idara ya maendeleo ya jamii Wilaya.

Mratibu alibainisha baadhi ya Tuzo zitakazo tolewa ni, Tuzo ya mkulima bora wa Bustani, Mkulima bora wa mazao ya biashara, mfugaji bora wa kuku, mfugaji bora wa ng’ombe, mfugaji bora wa nguruwe n.k
Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc