Mwalimu akutwa mtupu Shuleni Lindi
Akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake mwalimu wa taaluma wa shule hiyo, Francis Milanzi alisema walimu shuleni hapo wamekosa amani na kuwasababishia kuzihama nyumba zao kwa muda na badala yake kwenda kukesha kwenye ofisi za walimu tangu tukio hilo litokee.
Ofisa elimu wa Wilaya ya Lindi, Cosmas Magigi
alisema amepokea taarifa za tukio hilo kwa huzuni na amewaomba walimu
kuwa na subira wakati utaratibu wanalishughulikia suala hilo.
Magigi aliongeza kuwa ofisi yake itafanya
utaratibu wa kumhamisha mwalimu huyo na kumtafutia shule nyingine huku
akiwataka wakazi wa eneo hilo kujenga ushirikiano na watumishi ili
waweze kutekeleza majukumu yao.
Hili ni tukio la pili kutokea katika halmashauri
hiyo mwaka huu ambapo la kwanza lilitokea April katika Shule ya
Sekondari Ruhokwe, mwalimu wa shule hiyo alilazwa kwenye kibao cha
shule akiwa uchi wa mnyama.
http://youthforchang.blogspot.com/
Massawe ambaye anamiliki majumba na biashara ya
utalii katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba
alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti
wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe.
http://youthforchang.blogspot.com/
Interpol yamtia mbaroni Alex Massawe Dubai
http://youthforchang.blogspot.com/
Kwa ufupi
Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa
(Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav
Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya
Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai
akitokea Afrika Kusini.
“Maofisa wa Usalama wa uwanja wa ndege walimuuliza
kuwa wewe ndiye Alex Massawe? Alikana lakini alielezwa kuwa alama za
vidole vinaonyesha anaitwa hivyo,” kilidokeza chanzo cha habari hizi kwa
simu kutoka Dubai. Hata hivyo, Babile alisema hakuwa na taarifa za
Massawe kukutwa na pasi bandia za kusafiria.
Uvumi wa Aprili
Mapema Aprili 27, mwaka huu kulikuwa na habari
kwamba Massawe amekamatwa katika mji mmojawapo ulioko katika Pwani ya
Afrika Kusini.
Habari hizo za kukamatwa kwa Massawe, ambaye pia
hufadhili masuala ya kisiasa na michezo, zilisambaa kupitia mitandao
mbalimbali ya kijamii ya Facebook, Twitter na Jamii Forum. Kulikuwa kuna
mkanganyiko wa taarifa huku wengine wakidai alinaswa akiwa ndani ya
boti huko Afrika Kusini, wengine wakidai alikamatwa wakati akijaribu
kuingia Msumbiji akitokea Malawi.
Akizungumzia hilo Babile alisema huo ulikuwa ni
uzushi na baada ya kuzisikia taarifa hizo walifuatilia katika maeneo
aliyohusishwa kukamatwa na kubaini kwamba hapakuwa na ukweli wowote.