Home » » Mafunzo ya Nanenae Yawafurahisha Wakulima

Mafunzo ya Nanenae Yawafurahisha Wakulima

Wakulima wamefurahia mafunzo mbalimbali ya kuendesha  kilimo  yaliyokuwa yanatolewa katika maonyesho ya wakulima Nane Nane yaliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma.
Wakulima hao, waliongeza kuwa licha ya kujifunza mambo mbalimbali pia wameweza kupata mbembejeo za Kilimo kwa bei nafuu na kwa urahisi.
Alisema wakulima wameweza kujifunza mambo mbalimbali katika mashamba darasa yaliyoandaliwa na maofisa Kilimo kama mfano kwa wakulima waliokuja katika maonyesho hayo.
“Nimefurahia sana maonyesho hayo kwani yameniwezesha kupata pembejeo kama vile mtambo wa kupukuchi mahindi (global cycle solution) ambao unazwa kwa bei nafuu”, alisema Bwana Alex Sori mkulima wa mahindi kutoka Hombolo.
“Kwa kweli maonyesho haya yameniwezesha kujivunza vitu mbalimbali na jisi ya kukufanya Kilimo changu kuwa cha kisasa zaidi, nimejifunza aina mbalimbali za mbegu na jisi ya kuzipanda ili kuniwezesha kuweza kuvuna mzao mengi”, alisema Bwana Edwini Makaya mkulima kutoka wilayani Chamwino.
Aliongeza kuwa wameweza kujifunza aina mbalimbali za mbegu na jisi ya kupnda katika utaalaamu ambao utawawezesha kuvuna mazao mengi yatakoayoweza kuwaongezea kipata chao.
Bwana Sori aliwashauri wakulima kujenga tabia ya kutembelea maonyesho hayo kwani watawawezesha  kupata mbegu bora na kwa bei nafuu.
Pia alisema kupitia maonyesho hayo ameweza kujifunza teknolojia mbalmbli ambazo ni za kisasa kama vile Kilimo cha umwagiliaji na jinsi ya kutumia zana bora za Kilimo zikiwemo matrekta.
“Hakika maonyesho haya yamenipatia elimu ya namna ya kutumia zana mbalimbali za Kilimo ambazo nimekuwa sijawahi hata kiziona na nilizokuwa nazisikia, leo hii niomeweza kuziona kwa macho yangu na kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuzitumia”, alisema Bibi Magreti Haule, mkulima kutoka Wilayani Kongwa.
Katika maonyesho hayo wakulima pia waliweza kujifunza jinsi ya kudhibiti waduu waharibifu katika mazao mbalimbali kwa kutumia madawa ili kupunguza uharibifu wa mazao.

Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc