Home » » DC NZEGA APANIA KUWEZESHA VIJANA WAJIAJIRI

DC NZEGA APANIA KUWEZESHA VIJANA WAJIAJIRI



Mh. Mkuu wa Wilaya ya Nzega BITUNI MSANGI ameweka mikakati maalumu ya kuwezesha vijana walio katika mpango wa YOUTH FOR CHANGE kujiajiri kutokana na fursa za Kilimo na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hususani katika mpango wa miaka mitatu wa Serikali katika kuzalisha ajira Laki sita.
Akizungumza na Viongozi wa Youth for Change hivi karibuni Ofisini kwake, mara baada ya kurudi kutoka katika Semina elekezi iliyo andaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda juu ya usimamizi wa Miradi Sita ambayo ni kipau mbele cha Serikali katika mwaka huu wa Bajeti 2013/2014, alisema Vijana ni budi wakachangamkia fursa iliyotolewa na Serikali juu ya Kujikita katika katika Kilimo cha Biashara ili kujikwamua.
Alisema, vijana walio katika mpango wa kuwezesha vijana kujiajiri maarufu kama Youth for Change-Nzega, wameonesha mfano mzuri kwa wao kujitambua na kuanza hivyo Ofisi yake na Halmashauri ya Nzega kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii watatoa ushirikiano mkubwa ili kuhakikisha vijana wanafanikiwa katika mpango wao wa kujiajiri.
Aidha, alisema hivi sasa kila kijana asiye na ajira hususani vijana wasomi walio hitimu elimu ya juu, walioko katika Wilaya yake wanapaswa kujiunga katika mpango huo ili kwa pamoja waweze kujikita katika kilimo cha biashara sehemu ambayo itazalisha ajira nyingi zaidi kwa vijana wa mijini na vijijini.
Tayari katika mpango wa vijana Youth for Change alisha toa eneo kwa ajili ya kilimo katika Kijiji cha Upambo Kata ya ISANZU Wilayani Nzega lenye heka takribani 700, na vijana tayari wamejipanga kwa ajiri ya kuanza kilimo cha bustani hivi karibuni wakati wakisubiri musimu wa kilimo hapo mwezi wa kumi na moja.
Mh. Mkuu wa Wilaya ameweka mikakati mizuri katika kuhakikisha vijana hao wanafanikiwa ikiwemo mbinu mbalimbali za kutafuta fedha zitakazo saidia kufanya uwekezaji huwo wa Kilimo. Kwa upande wa ufugaji wa Nyuki, Bituni Msangi, alisema kuna aja ya kupata mizinga kwa haraka ili kuweza kuanza kwani ufugaji wa Nyuki ni rahisi na unafaida kubwa kutokana na asali ya Tabora kupendwa na watu wengi hapa nchini na nje ya nchi.
Naye Mratibu wa Mpango wa Youth for Change Ndugu. Boniphace Nyabweta, alisema vijana walio katika mpango wa YFC wamejipanga vizuri kwani tayari walisha wezeshawa mafunzo ya katika awafu mbili na taasisi inayo ratibu mpango huo INFORMATION FOR DISSEMINATION NETWORK na GIVE OPPORTUNITY.
Alisema katika awamu ya kwanza taasisi zinazo ratibu mpango ziliwawezesha vijana mafunzo juu ya Ujasiriamali, Afya, Rushwa na Matumizi ya Madawa ya Kulevya yaliyo tolewa na wakufunzi toka katika Idara mbalimbali za Serikali na Shirika la Kazi Duniani (ILO). Aidha katika awamu ya pili vijna waliwezeshwa katika mafunzo ya wiki moja ya Ujasiriamali ili waweze kuwa na ufahamu juu ya mbinu za kibiashara.
Share this article :
 
Support : Swahiliclan | harold | 0752490120
Copyright © 2011. YOUTH FOR CHANGE - All Rights Reserved
Template Created by swahiliclan Published by hashork
Proudly powered by sc